Wednesday, 10 June 2015

tazama Waganda wanavyopenda ngono mchana . Waziri wa maadili atoa tamko .



 
 
 

Matamshi ya waziri wa maadili nchini Uganda kuwa Waganda wengi hujihusisha na vitendo vya kufanya mapenzi hasa wakati wa kipindi cha mlo wa mchana yamezua gumzo kali katika vyombo vya habari nchini humo na katika mitandao ya kijamii.
Simon Lokodo ameongeza kusema wamiliki wa nyumba za kulala wageni wakamatwe kwa kuwaruhusu wafanyi kazi wanaotoka maofisini wakati wa mchana na kwenda kula uroda vyumbani humo.
Wengi wanakiri kuwa tetesi hizo zimeenea nchini humo kwamba wengi wa wafanyikazi hutumia fursa ya mapumziko ya mchana kujihusisha na vitendo vya ngono na makahaba au wapenzi wao wa pembeni.
Baadhi wanaunga mkono kauli hiyo ya waziri lakini wengine wamemtaka asijihusishe na maisha ya wengine

No comments:

Post a Comment

CAF kumuunga mkono INFANTINO Urais wa FIFA

Shirikisho la soka barani Afrika CAF linamuunga mkono Infantino Rais wa shirikisho la soka barani Africa (CAF) AHMAD AHMAD amesema shir...