Friday, 28 August 2015

Wahamiaji 71 wafariki kwenye Lori huko nchini Austria



Image copyright4 news
Image captionLori lililokuwa na miili ya wahamiaji
Maafisa wa polisi nchini Austria, wamethibitisha kuwa miili ya wahamiaji 71, imepatikana ndani ya lori moja iliyokuwa imeachwa kwenye barabara kuu.
Miili hiyo inajumuisha 59 ya wanaume, 8 ya wanawake na watoto wanne.
Msemaji wa polisi amesema kuwa wao wanashuku kuwa wahamiaji hao wanatoka nchini Syria.
Ameongeza kuwa watu watatu wamekamata nchini humo kuhusiana na vifo hivyo.
Wawili kati yao wakisiwa kuwa raia wa Bulgaria na mwiinge ni raia wa Bulgaria mwenye asili ya Lebabon
Waziri wa masuala ya ndani amesema tukio hilo linaashiria umuhimu wa suala la uhamiaji kushughulikiwa kwa dharura na viongozi wa Muungano wa Ulaya EU.
Miili hiyo imepatikana wakati viongozi wa Ujerumani ,Austria na nchi sita za mashariki mwa visiwa vya Balkan, wakikutana mjini Vienna kuzungumzia tatizo la uhamiaji.
Kansella wa Ujerumani Angela Merkel, amesema viongozi hao wamesikitishwa na ripoti hiyo.
Image copyright
Image captionKambi ya wahamiaji Austria
Amesema tukio hilo ni onyo kwa mataifa ya Ulaya kwamba swala la uhamiaji linaweza tu kutatuliwa iwapo kutakuwa na ushirikiano na uwajibikaji.
Nchi za ulaya zinazopokea idadi kubwa wahamiaji zimeonya kuwa iwapo nchi zingine hazitakubali kuwapa hifadhi wahamiaji athari za haua hiyo zitashuhudiwa katika Jumuiya nzima ya Ulaya.

No comments:

Post a Comment

CAF kumuunga mkono INFANTINO Urais wa FIFA

Shirikisho la soka barani Afrika CAF linamuunga mkono Infantino Rais wa shirikisho la soka barani Africa (CAF) AHMAD AHMAD amesema shir...