Sunday, 8 May 2016

Majonzi: Watu zaidi ya 73 watekea katika ajali mbaya Afghanistan


Image copyright
Image caption Abiria 73 wametekea hadi kufa katika ajali mbaya iliyohusisha mabasi mawili ya uchukuzi wa umma na lori la kubeba mafuta nchini Afghanistan.
Abiria 73 wametekea hadi kufa katika ajali mbaya iliyohusisha mabasi mawili ya uchukuzi wa umma na lori la kubeba mafuta nchini Afghanistan.
Msemaji wa wizara ya afya alieleza kuwa watu kama 70 walikufa...na kwamba wengi waliteketea na hawatoweza kutambulika.

Image copyright
Image caption Abiri wengine walipelekwa hospitalini katika jimbo la Ghazni.
Wakuu wa Afghanistan wanasema kuwa idadi inazidi kuongezeka ya watu waliokufa katika ajali hilo lililotokea katika barabara ya mji mkuu wa Kabul kuelekea mji ulioko kusini wa Kandahar.
Abiri wengine walipelekwa hospitalini katika jimbo la Ghazni.

Image copyright EPA
Image caption Mohammadullah Ahmadi, mkurugenzi wa trafiki wa mkoa huo analaumu utundu wa madereva kwa ajali hiyo.
Ajali za barabarani ni kawaida nchini Afghanistan ambapo madereva wanamazowea ya kukaidi kanuni za barabarani na pia maafisa wa kuelekeza magari ni mwachache mno.
Mwandishi wa BBC aliyeko huko Mahfouz Zubaide anasema kuwa magari hayo matatu yalikuwa yanaendeshwa kwa kasi mno.

Image copyright
Image caption Ajali za barabarani ni kawaida nchini Afghanistan ambapo madereva wanamazowea ya kukaidi kanuni za barabarani
Mohammadullah Ahmadi, mkurugenzi wa trafiki wa mkoa huo analaumu utundu wa madereva kwa ajali hiyo.
Anasema kuwa kwa jumla kulikuwa na abiria 125 katika mabasi hayo mawili.

Image copyright AFP
Image caption Anasema kuwa kwa jumla kulikuwa na abiria 125 katika mabasi hayo mawili.
Msemaji wa idara ya afya Ismail Kawasi anasema kuwa itakuwa vigumu kuwatambua kwani walioteketea ,waliteketea kabisa.

No comments:

Post a Comment

CAF kumuunga mkono INFANTINO Urais wa FIFA

Shirikisho la soka barani Afrika CAF linamuunga mkono Infantino Rais wa shirikisho la soka barani Africa (CAF) AHMAD AHMAD amesema shir...