Wednesday, 29 June 2016

Watu zaidi ya 36 wauawa Uturuki



Image copyrightGETTY
Image captionWatu 36 wauawa Uturuki
Watu 36 wameuawa katika shambulio la kujitoa muhanga katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Ataturk Istanbul nchini Uturuki,na wengine zaidi ya 100 kujeruhiwa
Shughuli za usafirishaji katika uwanja huo zimesitishwa huku shughuli ya uokoaji na huduma ya kwanza vikiendelea..
Gavana wa mji wa Istanbul amethibisha kuuawa watu hao 32 na idadi hiyo ya majeruhi.
Image copyrightREUTERS
Image captionLango la uwanja wa ndege
Mashuhuda wanasema waliwaona washambuliaji watatu,ambapo mmoja kati yao alikuwa akifyatua risasi kabla ya kujitoa muhanga kwa kujilipua kwa bomu na kufa.
Hata hivyo mashambulizi hayo yalihusisha katika eneo la kuingia katika uwanja huo.
Rais wa Uturuk Recep Tayyip Erdogan amelaani shambulio hilo na kusisitiza umoja katika kutokomeza vitendo hivyo.
Uturuki imekuwa ikikabiliwa na mashambulizi ya kigaidi kutoka pande mbili,kwanza kutoka kwa kundi la Islamic State wanaoingia kutoka nchi jirani ya Syria na waasi wa Kikurud wanataka kuunda dola yao.

vyama vya Upinzani Tanzania watishia kumshtaki rais Magufuli ICC uholanzi

File:Chadema bendera.jpg
Polisi katika kisiwa cha Pemba visiwani Zanzabar nchini Tanzania imepinga vikali kuwa inavunja haki za binadamu kwa kuwatesa na kuwashikilia wapinzani.
Hata hivyo limekiri kuwashikilia baadhi ya wapinzani kwa madai kwamba ni wahalifu.
Hapo jana Muungano wa Upinzani nchini Tanzania ulitoa kauli ya kulaani Polisi huko Pemba kwamba imekuwa ikiwapiga, kuwatesa na kuwafungulia kesi za bandia wafuasi wa upinzani .
Muungano huo tayari umetishia kumpeleka Rais wa Tanzania John Magufuli kwenye mahakama ya kimataifa ya ICC iwapo hataingilia kati mgogoro huo unaoendelea visiwani humo.
Kutoka Dar es Salaam mwandishi wetu Regina Mziwanda amezungumza na Naibu Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai wa Polisi Zanzibar Salum Msangi na kwanza alimuuliza hali ya usalama ikoje huko Pemba.

Baada ya kujitoa EU uingereza yapata pigo.



Image captionMuungano wa Ulaya

Uingereza imezuia kuhudhuria mkutano wa viongozi wa Jumuiya ya Ulaya ambapo itakuwa mara ya kwanza kufanyiwa hivyo kwa miaka 40.
Waziri Mkuu, David Cameron, hatakuwa mezani wakati viongozi wengine 27 wa mataifa wanachama wa Jumuiya ya Ulaya watakuwa wakihudhuria mkutano usio rasmi juu ya hatma ya muungano huo baada ya kuondoka kwa Uingereza.
Uingereza imeambiwa ianzishe mpango wake wa kuondoka katika jumuiya hiyo bila kuchelewa.
Rais wa Jumuiya ya Ulaya, Jean-Claude Junker, amesema kuwa shughuli za kutegua kujiondoa kwa Uingereza kutoka muungano huo zinapaswa kutekelezwa mara tu Uingereza inapompata Waziri Mkuu mpya.

Tuesday, 28 June 2016

Neema kubwa: Hifadhi kubwa zaidi ya gesi ya Helium yagunduliwa Tanzania



Image captionHifadhi kubwa zaidi ya gesi ya Helium yagunduliwa Tanzania
Tanzania ni miongoni mwa mataifa machache duniani yaliyojaliwa kuwa na rasilimali na madini mengi.
Na baada ya kugunduliwa kwa gesi asili huko Mtwara na dhahabu sasa watafiti kutoka Uingereza wamegundua hifadhi kubwa zaidi duniani ya gesi adimu zaidi ya Helium nchini Tanzania.
Watafiti kutoka chuo kikuu cha Oxford na kile cha Durham kwa ushirikiano na wataalumu wa madini kutoka Norway wamegundua uwepo wa takriban futi bilioni 54 za gesi hiyo ya barafu kama inavyofahamika.
Ugunduzi huo umefanyika katika eneo la bonde la ufa la Tanzania.
Katika taarifa kwa wanahabri huko Japan, watafiti hao wanasema kuwa uhaba wa gesi hiyo kote duniani ulikuwa umesababisha taharuki haswa kwa madaktari ambao wanatumia gesi hiyo adimu kuendesha mashine za utabibu zijulikanazo kama MRI scanners, mbali na kutumika katika mitambo ya kinyuklia miongoni mwa sekta zingine nyingi za kawi na teknolojia.
Kabla ugunduzi huo watafiti walikuwa wamebashiri ukosefu wa gesi hiyo baridi ifikapo mwaka wa 2035.
Image captionWataalumu wa madini kutoka Norway wamegundua uwepo wa takriban futi bilioni 54 za gesi hiyo ya barafu kama inavyofahamika.
Mnamo mwaka wa 2010 Mwanfisikia mshindi wa tuzo la Nobel Robert Richardson alikuwa ametabiri kumalizika kabisa kwa gesi hiyo.
Ukosefu huo ulikuwa umesababisha wataalamu kuhimiza kutungwa kwa sheria itakayopunguza matumizi yake katika bidhaa zisizo za dharura kama vile kwenye vibofu kutokana na hali ya kuwa gesi hiyo ya Helium ni nyepesi kuliko ile ya Oxygen.
''Gesi tuliyoipata huko Tanzania inaweza kujaza silinda za gesi milioni moja nukta 

Neema kubwa: Hifadhi kubwa zaidi ya gesi ya Helium yagunduliwa Tanzania



Image captionHifadhi kubwa zaidi ya gesi ya Helium yagunduliwa Tanzania
Tanzania ni miongoni mwa mataifa machache duniani yaliyojaliwa kuwa na rasilimali na madini mengi.
Na baada ya kugunduliwa kwa gesi asili huko Mtwara na dhahabu sasa watafiti kutoka Uingereza wamegundua hifadhi kubwa zaidi duniani ya gesi adimu zaidi ya Helium nchini Tanzania.
Watafiti kutoka chuo kikuu cha Oxford na kile cha Durham kwa ushirikiano na wataalumu wa madini kutoka Norway wamegundua uwepo wa takriban futi bilioni 54 za gesi hiyo ya barafu kama inavyofahamika.
Ugunduzi huo umefanyika katika eneo la bonde la ufa la Tanzania.
Katika taarifa kwa wanahabri huko Japan, watafiti hao wanasema kuwa uhaba wa gesi hiyo kote duniani ulikuwa umesababisha taharuki haswa kwa madaktari ambao wanatumia gesi hiyo adimu kuendesha mashine za utabibu zijulikanazo kama MRI scanners, mbali na kutumika katika mitambo ya kinyuklia miongoni mwa sekta zingine nyingi za kawi na teknolojia.
Kabla ugunduzi huo watafiti walikuwa wamebashiri ukosefu wa gesi hiyo baridi ifikapo mwaka wa 2035.
Image captionWataalumu wa madini kutoka Norway wamegundua uwepo wa takriban futi bilioni 54 za gesi hiyo ya barafu kama inavyofahamika.
Mnamo mwaka wa 2010 Mwanfisikia mshindi wa tuzo la Nobel Robert Richardson alikuwa ametabiri kumalizika kabisa kwa gesi hiyo.
Ukosefu huo ulikuwa umesababisha wataalamu kuhimiza kutungwa kwa sheria itakayopunguza matumizi yake katika bidhaa zisizo za dharura kama vile kwenye vibofu kutokana na hali ya kuwa gesi hiyo ya Helium ni nyepesi kuliko ile ya Oxygen.
''Gesi tuliyoipata huko Tanzania inaweza kujaza silinda za gesi milioni moja nukta 

Neema kubwa: Hifadhi kubwa zaidi ya gesi ya Helium yagunduliwa Tanzania



Image captionHifadhi kubwa zaidi ya gesi ya Helium yagunduliwa Tanzania
Tanzania ni miongoni mwa mataifa machache duniani yaliyojaliwa kuwa na rasilimali na madini mengi.
Na baada ya kugunduliwa kwa gesi asili huko Mtwara na dhahabu sasa watafiti kutoka Uingereza wamegundua hifadhi kubwa zaidi duniani ya gesi adimu zaidi ya Helium nchini Tanzania.
Watafiti kutoka chuo kikuu cha Oxford na kile cha Durham kwa ushirikiano na wataalumu wa madini kutoka Norway wamegundua uwepo wa takriban futi bilioni 54 za gesi hiyo ya barafu kama inavyofahamika.
Ugunduzi huo umefanyika katika eneo la bonde la ufa la Tanzania.
Katika taarifa kwa wanahabri huko Japan, watafiti hao wanasema kuwa uhaba wa gesi hiyo kote duniani ulikuwa umesababisha taharuki haswa kwa madaktari ambao wanatumia gesi hiyo adimu kuendesha mashine za utabibu zijulikanazo kama MRI scanners, mbali na kutumika katika mitambo ya kinyuklia miongoni mwa sekta zingine nyingi za kawi na teknolojia.
Kabla ugunduzi huo watafiti walikuwa wamebashiri ukosefu wa gesi hiyo baridi ifikapo mwaka wa 2035.
Image captionWataalumu wa madini kutoka Norway wamegundua uwepo wa takriban futi bilioni 54 za gesi hiyo ya barafu kama inavyofahamika.
Mnamo mwaka wa 2010 Mwanfisikia mshindi wa tuzo la Nobel Robert Richardson alikuwa ametabiri kumalizika kabisa kwa gesi hiyo.
Ukosefu huo ulikuwa umesababisha wataalamu kuhimiza kutungwa kwa sheria itakayopunguza matumizi yake katika bidhaa zisizo za dharura kama vile kwenye vibofu kutokana na hali ya kuwa gesi hiyo ya Helium ni nyepesi kuliko ile ya Oxygen.
''Gesi tuliyoipata huko Tanzania inaweza kujaza silinda za gesi milioni moja nukta 

Monday, 27 June 2016

Huyu hapa Black Coffee aliembwaga Diamond Platnumz BET,jua sababu hapa.


DJ raia wa Afrika Kusini ambaye pia ni producer maarufu kama Black Coffee, amewabwaga wanamuziki maarufu wakiwemo WizKid, Yemi Alade na Diamond Platnumz na kushinda tuzo la kimataifa la usanii la BET.
Mwaka uliopita Black Coffee alitoa albamu yake ya tano, Pieces of Me, na kupata mashabiki wengi.
Mwaka 2015 na 2016 umaarufu wake uling'aa katika ulingo wa kimataifa maeneo tofauti kote duniani
Tuzo hilo llitangazwa kupitia kwa mitandao ya kijamii.

Wednesday, 22 June 2016

Watu 30 wafariki dunia huko Libya hivi punde






Mapigano kati ya jeshi la Libya na wapiganaji wa Islamic State yamesababisha vifo vya zaidi ya watu 30.
Msemaji wa hospitali moja alisema kuwa wapiganaji 36 wameuawa huku wengine karibu 140 wakijeruhiwa katika mji wa Sirte ambao ni ngome ya Islamic state.
Wakati huo huo taarifa zinasema kuwa idadi ya watu waliouawa wakati mlipuko ulitokea katika ghala la silaha kwenye mji ulio magharibi wa Garabulli imeongezeka hadi watu 29.
Ghala hilo liliripotiwa kuwa ndani ya kambi inayotumiwa na wapiganaji kwenye mji wa Misrata pwani ya nchi.

Hatari: Korea Kaskazini yalipua makombora mengine.


Image copyrightAP
Image captionRais wa Korea Kaskazini Kim Jong Un
Korea Kusini inasema kuwa majirani zao Korea Kaskazini kwa mara nyingine tena, wameifanyia majaribio makombora yake mawili, hatua ya wazi ya kuonesha kukiuka hatua Umoja wa mataifa kuiwekea taifa hilo vikwazo vya kiuchumi. Taarifa zasema kombora la kwanza halikufanikiwa huku la pili likisafiri umbali wa kilomita mia nne.
Msemaji wa Waziri wa Umoja wa taifa wa Korea Kusini Joeng Joon-hee amesema majaribio hayo ni kukiuka vikwazo.
"Ulipuaji huo makombora kwa kutumia Teknolojia ya angani unakiuka maazimio ya Umoja wa mataifa. NIa ni uchokozi dhidi yetu. Tunashauri ni vyema kwa Korea Kaskazini kuzidisha nguvu katika kuimarisha amani katika eneo la rasi ya Korea na kwa maisha ya watu wake ambayo Korea kaskazini imekuwa ikisititiza kila wakati." Amesema
Naye waziri mkuu wa Japan Shinzo Abe amelaani hatua hiyo Korea ya Kaskazini.
"Leo kumelipuliwa makombora kwa kutumia teknolojia ya angani iliyotumika zamani huu ni ukiukwaji wa wazi wa azimio la Baraza la Usalama la Umoja wa mataifa. hatutarusu na tutaandaa azimio la kupinga hatua hiyo," amesema Waziri Mkuu huyo

Monday, 20 June 2016

nchi ya Urusi yapinga makubaliano ya kuumaliza ugomjwa wa UKIMWI


Symbolbild Aids

Umoja wa Mataifa umekubaliana kuongeza jitihada za kumaliza janga la UKIMWI, ifikapo mwaka 2030, ingawa Urusi imetaka kutowalenga zaidi watumiaji wa dawa za kulevya na wanaume wanaojihusisha na mapenzi ya jinsia moja.
Makubaliano hayo ya kisiasa yamefikiwa na wanachama 193 katika mkutano mkuu, ulioweka msisitizo juu ya mahitaji ya kuwasaidia wanaotumia dawa za kulevya kwa kujidunga sindano, wanaojihusisha na biashara ya ngono, wanaobadilisha jinsia na wafungwa amabo wapo katika hatari kubwa ya kupata maambukizi ya virus UKIMWI.
Maambukizo ya Virusi vya UKIMWI yamekuwa yakipungua katika muongo mmoja uliopita, lakini bado kuna kiasi ya watu Milioni 36.7 duniani kote wanaoishi na Virusi vya UKIMWI ama UKIMWI, na wengi wao wakiwa katika eneo la Kusini mwa Jangwa la Sahara, ambako Mkurugenzi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia UKIMWI, UNAIDS, Michel Sidibe amesema ndiko kuna idadi kubwa ya watu wanaotumia dawa.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-moon amewaambia wajumbe wa mkutano huo kwamba UKIMWI bado ni tishio, kwa hiyo mataifa bado yana nafasi ya kuhakikisha yanabadilisha hali ya janga hilo katika kipindi cha miaka mitano ijayo.
Ban ametaka kutolewa kwa huduma na dawa kwa watu wote wanaoishi na Virusi vya UKIMWI bila ya ubaguzi. Aliwalenga zaidi vijana wadogo, wahamiaji, wanawake na wasichana, wanaofanya biashara ya ngono, wanaume wanaojihusisha na mapenzi ya jinsia moja, wanaojidunga dawa za kulevya, wanaobadilisha maumbile na wafungwa.
Mkurugenzi Mtendaji wa UNAIDS,Michel Sidibe amesema idadi ya watumiaji dawa Barani Afrika inaridhisha
Mkurugenzi Mtendaji wa UNAIDS, Michel Sidibe amesema idadi ya watumiaji dawa Barani Afrika inaridhisha
Makubaliano haya yanatokana na mipango ya awali ya Umoja wa Mataifa kuhusu UKIMWI yaliyopitishwa miaka mitano iliyopita, kwa kuweka msisitizo zaidi kwa kwale walioko kwenye hatari kubwa ya kupata maambukizi. Makubaliano hayo yamelenga maeneo matatu yanayootakiwa kufikiwa ifikapo mwaka 2020, ambayo ni kupunguza maambukizi mapya ya Virus vya UKIMWI, kupunguza idadi ya vifo na kuondoa unyanyapaa dhidi ya watu wanaoishi na Virusi vya UKIMWI.
Urusi ilitaka mabadiliko ya mkakati huo mpya kuangazia sheria za kitaifa na namna zinavyoyataja makundi ya wanaume wanaojihusisha na mapenzi ya jinsia moja, watumiaji wa dawa za kulevya na wafungwa. Walisema wanadiplomasia na makundi ya kiraia, Jumanne hii.
Mabadiliko hayo yalipingwa vikali kutokana na hofu kwamba yataruhusu Urusi, Iran na nchi nyingine zinazochukulia mapenzi ya jinsia moja kama uhalifu kuzuia dawa za kupunguza makali ya UKIMWI na huduma nyingine kwa wanaume hao.
Mkutano huo wa siku tatu, ulianza kwa ombi la mjukuu wa aliyekuwa Rais wa Afrika Kusini, Nelson Mandela, Indaba ambaye baba yake alikufa kwa UKIMWI mwaka 2005, akiwataka viongozi wa nchi 35 zinazozuia watu walioathirika kuingia nchini mwao, ikiwa ni pamoja na Urusi na Singapore kuondoa marufuku hiyo.

kikundi cha Al shabaab chawaua polisi 5 Mandera Kenya hivi punde.


Image copyrightAP
Image captionAl shabaab waua polisi 5 Mandera Kenya
Maafisa 5 wa polisi wa Kenya wameuawa mapema leo mjini Mandera katika shambulizi lililotekelezwa na wapiganaji wa kundi la wanamgambo la Al shabab kutoka Somalia.
Kamishna wa jimbo hilo la kaskazini mashariki mwa Kenya bwana Job Borongo ameithibitishia BBC kuwa wapiganaji hao walifanya shambulizi la kuvizia dhidi ya msafara wa magari ya polisi uliokuwa ukienda El Wak wakitumia guruneti.
Maafisa hao tano waliangamia papo hapo huku gari walimokuwa wakisafiria likiharibiwa kabisa.
Maafisa wengine wanne wamejeruhiwa vibaya.
Msafara huo wa polisi ulikuwa ukitoa ulinzi kwa msafara wa mabasi ya uchukuzi wa umma, desturi iliyoanzishwa baada ya wapiganaji hao kuteka basi moja na kuua abiria 28 wakristu.
Gavana wa Mandera bwana Ali Roba aliwalaumu maafisa wa polisi katika eneo hilo kwa kupuuza tahadhari iliyotolewa na wenyeji kuhusiana na mashambulio ya kigaidi.
Image copyright
Image captionMaafisa hao tano waliangamia papo hapo huku gari walimokuwa wakisafiria likiharibiwa kabisa.
Roba anasema walipuuza vyanzo vya kiintelijensia vilivyotolewa kuhusiana na kuonekana kwa wapiganaji hao waliojihami.
Hii si mara ya kwanza Mandera kushuhudia mashambulizi ya al shabaab.
Shambulizi hilo la Novemba mwaka wa 2014 liliwaacha wasafiri wengi wasiokuwa waislamu na hofu ya kusafiri na hivyo kuilazimu serikali kutoa usalama kwa mabasi ya uchukuzi wa umma.
Mwezi mmoja baadaye wapiganaji hao waliwaua wachimba migodi 36 katika eneo hilo la Mandera.
Kundi hilo la wapiganaji wa kiislamu limekuwa likitekeleza mashambulizi katika maeneo ya kaskazini mwa Kenya likitaka kuishinikiza taifa hilo jirani kuondoa majeshi yake nchini Somalia.
Image captionGavana wa Mandera bwana Ali Roba aliwalaumu maafisa wa polisi katika eneo hilo kwa kupuuza tahadhari iliyotolewa na wenyeji
Kenya ilipeleka vikosi vyake vya jeshi nchini Somalia mwaka wa 2011 ikitaka kuzima mashambulizi ya mara kwa mara.
Hata hivyo kundi hilo limeongeza mashambulizi nchini kenya ikiwemo mauaji ya watu 67 katika maduka ya Westgate mjini Nairobi mwaka wa 2013.
Mwaka uliopita Al Shabab ilitekeleza mashambulizi katika chuo kikuu cha Garissa na kusababisha vifo vya wanafunzi 148

Friday, 17 June 2016

Auawa akichuma kuvu dawa ya 'nguvu za kiume



A'

  • Saa 9 zilizopita
Image copyrightAP
Image caption
Mtu mmoja amepigwa risasi na kuuawa katika kijiji cha Nepal alipokuwa akichuma kuvu fulani inayotambuliwa kwa uwezo wake wa kuongeza nguvu za kiume.
Kuvu hiyo inayotambulika kama ''Himalayan Viagra'' inasemekana kuwaongezea ashki walaji wake.
Kuvu hiyo ni kitega uchumi cha wenye vijiji wa maeneo ya milimani.
Haijulikani kwanini genge hilo la wavamizi liliwashambulia watu hao waliokuwa wakichuma kuvu hiyo katika wilaya ya mugu ila maafisa wa utawala wamethibitisha kuwa watu wengine watatu walijeruhiwa katika shambulizi hilo.
Ukungu au kuvu hiyo humea kwenye mwili wa nondo au mtoto wa kipepeo na kilo moja ya kuvu hiyo inaweza kuuza kwa maelfu ya dola za Marekani nchini Uchina.
Image captionAuawa akichuma kuvu yenye 'nguvu za kiume'
Biashara hiyo ni mojawapo ya njia ambazo raia wengi masikini wa jamii zinazoishi katika maeneo ya milima ya Hilamaya hujipatia riziki.
Kila mwaka maelfu ya watu kutoka vijijini hufunga safari kwa kutumia nyumbu na ngombe hadi maeneo ya milimani kutafuta ukungu huo unaomea kwenye mwili wa nondo.
Wakati wa msimu wa mavuna, shule hata hufungwa ili wanafunzi wawasaidie wazazi wao kutafuta kuvu.
Hii sio mara ya kwanza kwa ghasia kutokea katika eneo hilo.
Mwaka wa 2009 watu saba waliuawa baada ya mzozo kutokea kuhusu hati miliki ya kutafuta ukungu huo katika maeneo ya milima.
Licha ya utajiri unaotokana na mauzo ya ukungu, raia wengi nchini humo wanaiona kuwepo kwake kama laana kubwa kwa jamii.

CAF kumuunga mkono INFANTINO Urais wa FIFA

Shirikisho la soka barani Afrika CAF linamuunga mkono Infantino Rais wa shirikisho la soka barani Africa (CAF) AHMAD AHMAD amesema shir...