Monday, 1 October 2018

HAMILTON akaribia taji la 5 la dunia


Dereva wa kampuni ya FERARI, SEBASTIAN VERTEL anasema bado ana nafasi ya kushinda taji la mbio za langalanga msimu huu licha ya kuachwa kwa tofauti ya alama 50 na mpinzani wake mkubwa LEWIS HAMILTON. 

 HAMILTON amejiweka katika nafasi nzuri ya kushinda taji la TANO la mbio za langalanga baada ya kuibuka kinara katika michuano ya RUSSIAN GRAND PRI iliyofanyika mjini SOCHI. 

Ushindi huo unamfanya HAMILTON kufikisha alama 306 katika nafasi ya kwanza kwenye msimao huku VERTAL akiwa katika nafasi ya pili akiwa na alama 256 na VERTAL anasema anajua si kazi rahisi kupindua matokeo hayo lakini atafanya kila analoweza kuwashangaza wengi mwisho wa msimu.



Mpaka sasa yamebaki mashindano MATANO kukamilisha msimu ambayo ni pamoja na yale ya huko SUZUKA, JAPAN yatakayofanyika OCTOBA 7, mashindano ya MAREKANI yatakayofanyika OCTOBA 21mjini AUSTIN, mashindano ya MEXICO mjini MEXICO CITY, OCTOBA 28, BRAZIL mjini SAO PAULO, NOVEMBA 11 na yale yatakayofanyika mjini YAS MARINA huko ABU DHABI, NOVEMBA 25.   

No comments:

Post a Comment

CAF kumuunga mkono INFANTINO Urais wa FIFA

Shirikisho la soka barani Afrika CAF linamuunga mkono Infantino Rais wa shirikisho la soka barani Africa (CAF) AHMAD AHMAD amesema shir...