Credits to millady ayo
Sunday, 22 June 2014
Saturday, 21 June 2014
Thursday, 19 June 2014
RAISI MSHTAKIWA WA SIERRA LEONE CHARLES TAYLOR APINGA KUTUMIKIA KIFUNGO UINGEREZA
Rais wa zamani wa Liberia, ameanzisha harakati za
kisheria kupinga amri ya kutumikia kifungo chake cha jela
nchini Uingereza.
Taylor alifungwa jela kwa uhalifu dhidi ya binadamu na anakataa
kutumikia kifungo hicho Uingereza akisema kuwa ananyimwa
haki ya kufurahia maisha yake.
Charles Tayor anatumikia kifungo cha miaka hamsini jela kwa
makosa ya ubakaji na kutumia watoto kama wanajeshi wakati
wa vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini Sierra Leone.
Mawakili wake wanasema kuwa kuzuiliwa kwake nchini
Uingereza kunakiuka haki za binadamu kwa sababu ni mbali
sana na yumbani kwa familia yake kuweza kusafiri huko
kumuona.
Wanasema kuwa badala ya kutumikia kifungo Uingereza,
aruhusiwe kutumikia kifungo hicho nchini Rwanda, pamoja na
wafungwa wengine waliohukumiwa na mahakama maalum ya
umoja wa mataifa kuhusu Sierra Leone.
Pia wanasema anahofia kushambuliwa na wafungwa wengine
katika gereza la Frankland, Kaskazini mwa Uingereza.
MAREKANI SASA YAIWEKEA UGANDA VIKWAZO VIKALI BAADA YA KUPINGA SERA YA USHOGA
Afisa wa mahusiano anayesimamia maswala ya usalama katika
ikulu ya whitehouse Caitlin Hayden anasema kupitia kwa barua
kwa wanahabari kuwa sheria hiyo iliyopitishwa na bunge la
Uganda mwezi Februari inakiuka haki za binadamu.
Vikwazo hivyo vitajumuishwa marufuku ya wanaharakati
waliopigia debe sheria hiyo kupitishwa kutoingia Marekani.
Miradi itakayoathirika na marufuku hiyo ni pamoja na
ushirikiano na polisi wa Uganda Wizara ya Afya.
Sekta ya Afya na usalama wa taifa itaathirika na vikwazo hivyo.
Aidha msaada kwa miradi iliyoanzishwa kwa usaidizi wa
marekani pia utapunguzwa mbali na kufutiliwa mbali kwa
mazoezi ya kijeshi kati ya majeshi ya uganda na yale ya
Marekani.
Sheria hiyo inaharamisha uhusiano baina ya watu wa jinsia
moja na wale watakaopatikana wanaweza kuhukumiwa kifungo
cha maisha jela.
Hii ndiyo hatua ya hivi karibuni iliyochukuliwa na Marekani
katika ajenda yake ya kupinga sheria hiyo mpya nchini Uganda.
Juma lililopita Seneta mmoja kutoka Marekani ,Kirsten
Gillibrand alilalmikia vikali uteuzi wa waziri wa maswala ya
kigeni wa Uganda Sam Kutesa kuchaguliwa kuwa rais wa Umoja
wa Mataifa kutokana na kuwa anatokea Uganda.
Marekani imeiwekea Uganda vikwanzo kuhusina na sheria ya
wapenzi wa jinsia moja.
Watu 9000 walikuwa wametia sahihi pendekezo la kuitaka
Umoja wa Mataifa kumng'oa kitini bw Kutesa aliyechaguliwa
licha ya kampeini hiyo.
Wanaharakati wa wapenzi wa jinsia moja wameenda
mahakamani wakitaka sheria hiyo iondolewe lakini inatarajiwa
kupingwa kwani rais Yoweri Museveni aliupitisha maksudi
kudhihirishia wafuasi wake kuwa yu huru kutokana na shinikizo
kutoka kwa mataifa ya ughaibuni .
Punde baada ya kupitishia kwa sheria hiyo mpya benki kuu ya
dunia iliahirisha utoaji wa mkopo wa dola milioni 90 ambazo
zilikuwa zinapaswa kutumika kuimarisha sekta ya Afya nchini
Uganda .
Mataifa mengi tu ikiwemo Denmark, Norway, Uholanzi na
Sweden zote zimekatiza msaada kwa taifa hilo la Afrika
Mashariki.
CAF kumuunga mkono INFANTINO Urais wa FIFA
Shirikisho la soka barani Afrika CAF linamuunga mkono Infantino Rais wa shirikisho la soka barani Africa (CAF) AHMAD AHMAD amesema shir...

-
Tuzo za VMA 2014 zimefanyika na mastaa wengi walifika kwenye hilo tukio. Listi ya mastaa hao iliongozwa na familia ya Jay Z na Beyon...
-
Luca Modric mchezaji bora wa mwaka wa FIFA Wameamua kumpa,ni baada ya kumdhurumu tuzo yake ya msimu wa 2009/10,mwaka huu wameona ai...
-
Mlinda mlango wa Derby Country akipangua mkwaju wa Phil Jones Timu ya DERBY COUNTY inayonolewa na nyota wa zamani wa CHELSEA, FRANK LAM...