Tuesday, 30 June 2015
Monday, 29 June 2015
Sunday, 28 June 2015
Aliyejilipua Kuwait huyu hapa pichani, ni raia wa Saudi
Vyombo
vya habari nchini Kuwaiti zinasema kuwa mlipuaji wa kujitolea mhanga
aliyejilipua ndani ya msikiti nchini humo Ijumaa na kusababisha vifo vya
watu zaidi ya 25 ni raia wa Saudi Arabia.
Katika taarifa
iliyotolewa na wizara ya usalama wa ndani nchini Kuwait mshambuliaji
huyo anatambuliwa kuwa ni Fahd Suliman Abdul-Muhsen al-Qabaa.Yamkini taarifa hiyo inasema kuwa Fahd alikuwa ametua katika uwanja wa kimataifa wa ndege ulioko Kuwaiti saa chache kabla yake kutekeleza shambulizi hilo la kwanza kutokea nchini humo.
Kulingana na maafisa wa uhamiaji, Fahd alikuwa nchini humo kinyume cha sheria.
Kundi hilo linawakashifu waislmu washia kuwa wanakufuru na kukiuka maadili haswa na mafundisho ya mtume Muhammad.
Mashambulizi haya haswa kwa mataifa yanayochangia jeshi la muungano linalopigana na Wahouthi nchini Yemen na Islamic State nchini Syria na Iraq yamefikisha ujumbe wa ugaidi nyumbani kwa mataifa ya kanda hiyo ya ghuba kwa mujibu wa mwandishi wa BBC wa maswala ya Mashariki ya kati na ghuba Sebastian Usher.
Kuwait inaidadi kubwa ya washia katika kanda hiyo.
Saturday, 27 June 2015
lione gari alilopewa dogo aslay na mkubwa fella kama hukubahatika kuliona.
aslay kwa furaha kubwa akasema haya:
“Asante mungu Kwa kunipa uhai Na kipaji ambacho leo hii kina fanya naitwa Aslay pia nakushukuru kwa kunifikisha kwenye mikono Ya mtu mwenye moyo wa kibinaadamu. Najua kuna mengi makubwa ambayo boss wangu @mkubwafella umenifanyia ambayo si vyema kuyataja yote kwasababu wakati wake haujafikia ila naomba nichukue fulsa hii kukushukuru kwa hiki ulichonifanyia leo katika sherehe Ya kusherehekea siku yangu Ya kuzaliwa umenifanya nijione mwenye thamani kubwa duniani sikutegemea kama leo itakuwa siku yangu ya kumbukumbu ambayo sitoweza kuisahau hata Nije kuwa bilionea @mkubwafella asante kwa kunipa hii zawadi ambayo mimi kama mimi sikuiwazia kabisa kama Leo nitapata gari Na ninaushukuru uwongozi mziki Wa #mkubwanawanawe pamoja na manager wangu @chambusso boss wangu @babutale @mhtemba na mama yangu @sweatfella bila kuwasahau wasanii wenzangu wa @yamoto_band mungu

Mahakama Marekani yaruhusu ndoa za mashoga, ona wanavyoshangilia
Mahakama kuu nchini Marekani imetoa hukumu Ijumaa na kusema katiba ya
nchi hiyo inatoa haki kwa wapenzi wa jinsia moja kuoana, na hivyo kutoa
ushindi wa kihistoria kwa vuguvugu linalotetetea haki za mashoga.
Hukumu hiyo iliyopitishwa na majaji watano dhidi ya wanne imesema
uhakikisho wa katiba wa ulinzi sawa chini ya sheria unamaanisha kuwa
majimbo hayawezi kupiga marufuku ndoa za jinsia moja. Kufuatia hukumu
hiyo, ndoa za jinsia moja zitakuwa halali katika majimbo yote 50 ya
Marekani.
Jaji Anthony Kennedy, akiandika kwa niaba ya mahakama, amesema matumaini ya wapenzi wa jinsia moja wanaopanga kuoana ni kutengwa na kuishi maisha ya upweke, na kutenganishwa na taasisi za moja ya demokrasia za muda mrefu zaidi duniani. "Wanaomba heshima sawa mbele ya sheria. Katiba inawapa haki hiyo," amesema.
Kennedy ambaye hutoa kura ya maamuzi katika kesi katika kesi zenye mvuto mkubwa, aliungwa mkono na wengine wa majaji wanne waliberali wa mahaka hiyo. Kennedy ambaye aliteuliwa na rais Mrepublican Ronald Reagan mwaka 1988, hivi sasa ameandika hukumu zote muhimu nne kuhusu haki za mashoga, ambapo ya kwanza ilikuja mwaka 1996.
"Bila kutambuliwa, utulivu na kutabirika kwa ndoa, watoto wao watateseka na unyanyapa wa kujua kuw afamilia zao haziko sawa na nyingine," aliandika Kennedy. Katika maoni yanayokinzana, jaji mhafidhina Antonin Scalia, alisema uamuzi huo unaonyesha kuwa mahakama hiyo ni tishio kwa Wamarekani.
Jaji mkuu wa Marekani, mhafidhina John Roberts, alisoma muhtasari wa upinzani wake kutokea nje ya chemba la majaji, hii ikiwa mara ya kwanza kwake kufanya hivyo katika kipindi cha miaka 10 aliokaa katika mahakama hiyo. Roberts alisema ingawa zipo hoja za nguvu kisera katika suala la ndoa za jinsia moja, halikuw ajukumu la mahakama hiyo kuyalaazimisha majimbo kubadili sheria zake za ndoa.
Obama, Clinton washerehekea, Republican walaani
Rais Barack Obama, ambaye ni rais wa kwanza alieko madarakani kuunga mkono waziwazi ndoa za jinsia moja, alisifu hukumu hiyo, akisema kwenye mtandao wake wa twitter kuwa siku ya leo ni hatua muhimu katika safari ya kuhakikisha usawa kwa watu wote.
Naye Hillary Clinton, mgombea anaepewa nafasi kubwa kupitishwa na chama Demokratic kuwania urais mwaka 2016, aliandika kwenye mtandao wake wa twitter kuwa "Najivunia kusherehekea ushindi wa usawa wa ndoa." Hadi mwaka 2013, Clinton alisema alikuwa anapinga ndoa za jinsia moja, lakini alibadili mtazamamo wake tangu wakati huo.
Mgombea wa chama cha Republican Mike Hackabee alisema, uamuzi huu wa udanganyifu ni uababe wa mahakama unaokwenda kinyume na katiba." Mgombea mwingine wa Republican Jeb Bush aliongeza kuwa, " nikiongozwa na imani yangum naamini katika ndoa za asili. Naamini mahakama kuu ilipaswa kuyaruhusu majimbo yafanye uamuzi huu.
Ndoa za jinsia moja zilikuwa zinaruhusiwa katika majimbo 36 ya Marekani pamja na Washington DC. Katika jimbo la 37 la Alabama, mahakama iliondoa marufuku dhidi ya ndoa za jinsia moja, lakini mahakama ya rufaa iliwazuwia maafisa wa serikali kutoa leseni kwa wapenzi wa jinsia moja.
Wapinzani wa ndoa hizo wanasema uhalali wake unapaswa kuamuliwa na majimbo yenyewe, na wengine wanasema kuruhusiwa kwa ndoa hizo ni dharau kwa ndoa ya asili kati ya mwanamume na mwanamke, na kwamba Biblia inalaani mahusiano ya jinsia moja.
Hisia juu ya hilo zilikuwa juu wakati wa mjadala mahakamani mwezi April katika kesi hiyo, pale mwandamanaji alipowapigia kelele majaji na kuwambia wataozea jahanam ikiwa watapitisha hukumu kuunga mkono ndoa za jinsia moja.
Jaji Anthony Kennedy, akiandika kwa niaba ya mahakama, amesema matumaini ya wapenzi wa jinsia moja wanaopanga kuoana ni kutengwa na kuishi maisha ya upweke, na kutenganishwa na taasisi za moja ya demokrasia za muda mrefu zaidi duniani. "Wanaomba heshima sawa mbele ya sheria. Katiba inawapa haki hiyo," amesema.
Kennedy ambaye hutoa kura ya maamuzi katika kesi katika kesi zenye mvuto mkubwa, aliungwa mkono na wengine wa majaji wanne waliberali wa mahaka hiyo. Kennedy ambaye aliteuliwa na rais Mrepublican Ronald Reagan mwaka 1988, hivi sasa ameandika hukumu zote muhimu nne kuhusu haki za mashoga, ambapo ya kwanza ilikuja mwaka 1996.
"Bila kutambuliwa, utulivu na kutabirika kwa ndoa, watoto wao watateseka na unyanyapa wa kujua kuw afamilia zao haziko sawa na nyingine," aliandika Kennedy. Katika maoni yanayokinzana, jaji mhafidhina Antonin Scalia, alisema uamuzi huo unaonyesha kuwa mahakama hiyo ni tishio kwa Wamarekani.
Jaji mkuu wa Marekani, mhafidhina John Roberts, alisoma muhtasari wa upinzani wake kutokea nje ya chemba la majaji, hii ikiwa mara ya kwanza kwake kufanya hivyo katika kipindi cha miaka 10 aliokaa katika mahakama hiyo. Roberts alisema ingawa zipo hoja za nguvu kisera katika suala la ndoa za jinsia moja, halikuw ajukumu la mahakama hiyo kuyalaazimisha majimbo kubadili sheria zake za ndoa.
Obama, Clinton washerehekea, Republican walaani
Rais Barack Obama, ambaye ni rais wa kwanza alieko madarakani kuunga mkono waziwazi ndoa za jinsia moja, alisifu hukumu hiyo, akisema kwenye mtandao wake wa twitter kuwa siku ya leo ni hatua muhimu katika safari ya kuhakikisha usawa kwa watu wote.
Naye Hillary Clinton, mgombea anaepewa nafasi kubwa kupitishwa na chama Demokratic kuwania urais mwaka 2016, aliandika kwenye mtandao wake wa twitter kuwa "Najivunia kusherehekea ushindi wa usawa wa ndoa." Hadi mwaka 2013, Clinton alisema alikuwa anapinga ndoa za jinsia moja, lakini alibadili mtazamamo wake tangu wakati huo.
Mgombea wa chama cha Republican Mike Hackabee alisema, uamuzi huu wa udanganyifu ni uababe wa mahakama unaokwenda kinyume na katiba." Mgombea mwingine wa Republican Jeb Bush aliongeza kuwa, " nikiongozwa na imani yangum naamini katika ndoa za asili. Naamini mahakama kuu ilipaswa kuyaruhusu majimbo yafanye uamuzi huu.
Ndoa za jinsia moja zilikuwa zinaruhusiwa katika majimbo 36 ya Marekani pamja na Washington DC. Katika jimbo la 37 la Alabama, mahakama iliondoa marufuku dhidi ya ndoa za jinsia moja, lakini mahakama ya rufaa iliwazuwia maafisa wa serikali kutoa leseni kwa wapenzi wa jinsia moja.
Wapinzani wa ndoa hizo wanasema uhalali wake unapaswa kuamuliwa na majimbo yenyewe, na wengine wanasema kuruhusiwa kwa ndoa hizo ni dharau kwa ndoa ya asili kati ya mwanamume na mwanamke, na kwamba Biblia inalaani mahusiano ya jinsia moja.
Hisia juu ya hilo zilikuwa juu wakati wa mjadala mahakamani mwezi April katika kesi hiyo, pale mwandamanaji alipowapigia kelele majaji na kuwambia wataozea jahanam ikiwa watapitisha hukumu kuunga mkono ndoa za jinsia moja.
WATU 27 WAUWAWA KWA SHAMBULIO HUKO KUWAIT . ONA VIDEO NA PICHA YAKE HAPA
Maombolezi yanaendelea nchini kuwait kuwakumbuka watu 27 waliouawa kwenye shambulizi la kujitoa mhanga kwenye msikiti wa kishia.
Wakati
huo huo msemaji wa kampuni ya kitaifa ya mafuta nchini kuwait anasema
kuwa usalama umedumishwa katika vituo vyote vya mafuta kote nchuni humo
baada ya shambulizi ambalo Islamic State wanasema kuwa walihusika.Islamic State huwaita waislamu wa madhehebu wa shia kuwa wazushi na hivi majuzi walishambulia misikiti yao miwili katika nchi jirani ya Saudi Arabia.
Thursday, 25 June 2015
condom zinazotambua magonjwa zaja, zione hapa
Wanafunzi katika shule ya Isaac Newton Academy iliyoko Ilford, Uingereza wamezindua mipira ya kiume ‘kondomu’ yenye uwezo wa kugundua maradhi ya zinaa wakati watumiaji wanapokutana kimwili.
Kondomu hiyo inayojulikana kama S.T.EYE inabadili rangi pindi inapokutana na majimaji ya mtu anayeugua maradhi ya zinaa.
Kulingana na wanafunzi hao kondomu hiyo inabadili rangi tofauti kulingana na bakteria waliopo kwa muhusika.
Kutukana na kuvumbua mipira hiyo wanafunzi hao tayari wametunukiwa tuzo ya ubunifu na kampuni ya ubunifu wa kiteknolojia ya ‘the TeenTech’ pamoja na pauni 1,000.
Wanafunzi hao wamesema wameamua kufanya hivyo kwa lengo la kusaidia vizazi vijavyo ili kuepukana na maradhi yanayoweza kuzuilika kitaalam
.
.
Wednesday, 24 June 2015
watu 18 wafa huko china leo
Ripoti
za vyombo vya habari nchini Marekani zinasema kuwa watu 18 wameaga
dunia katika eneo la Uchina la Xinjiang katika makabiliano na polisi
katika eneo la ukaguzi.
Radio Free Asia inasema kuwa watu hao wa kabila la Uighurs walitumia visu na mabomu kuwashambulia maafisa wa polisi.Hakujakuwa na mawasiliano rasmi kuhusu tukio hilo lakini wafanyikazi wa hospitali katika mji wa Kashgar wameiambia BBC kuwa maafisa hao wa polisi walipokea matibabu.
Moja ya lengo huenda ni kuweka vikwazo vikali kwa waislamu wa Uighurs katika mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadan.
watu 120 wameuwa hivi punde huko mogadishu
Mogadishu Somalia
Mlipuaji wa kujitolea muhanga ameligongesha gari lake na lile la
kijeshi katika mji mkuu wa Somalia Mogadishu na kusababisha mlipuko
mkubwa.
Ripoti zinasema kwamba takriban watu 12 waliuawa na wengine kujeruhiwa wengi wakiwa raia.
Shambulizi hilo lilitokea karibu na ubalozi wa falme za kiarabu UAEVyombo vya habari nchini Somalia vimeripoti kwamba balozi amenusurika mlipuko huo ambao umeutaja kama jaribio la mauaji.
Tuesday, 23 June 2015
Joto kali lawaua watu 700 Pakistan
Waziri mkuu nchini Pakistan Nawaz Sharrif ametaka hatua za dharura kuchukuliwa huku idadi ya watu waliofariki kutokana na wimbi la joto katika mkoa wa kusini wa Sindh ikifikia 700.
Mamlaka ya kukabiliana na majanga ya dharura NDMA imesema kuwa imepokea maagizo kutoka kwa Nawaz Sharrif kuchukua hatua za dharura.
Jeshi tayari limepelekwa katika eneo hilo kujenga vituo vya kukabiliana na joto hilo ili kuisaidia mamlaka hiyo.
Wengi wa waathiriwa ni watu wazima kutoka kwa familia zinazopata mapato ya chini.
Maafisa wa afya wanasema vifo vingi vimetokea katika mji mkuu wa Karachi ambao ulikumbwa na joto la viwango vya juu vya hadi digree 45 c.
Katibu wa afya katika mkoa wa Sindh Saeed Mangnejo amesema kuwa watu 612 walifariki katika hospitali kuu ya serikali mji huo katika kipindi cha siku nne zilizopita.
Wengine 80 wameripotiwa kufariki katika hospitali za kibinafsi.
Sunday, 21 June 2015
Mapigano makali yaendelea Mogadishu
Mapigano makali yaendelea Mogadishu
Mapigano makubwa yameripotiwa kwenye mji kuu wa Somalia Mogadishu baada ya shambulizi la gari la kujitoa mhanga kutokea karibu na makao makuu ya idara ya ujasusi ya nchi hiyo.
Maafisa nchini Somalia wanasema kuwa wapiganaji kutoka kundi la al-Shabab waliingia jengo lililo karibu na makao hayo makuu ya ujasusi, na kukana madai ya al-Shabab kuwa waliingia makao ya ujasusi yenyewe.
Hakuna ripoti zozote zilizotolewa za watu kuuawa au kujeruhiwa
Al-Shabab wameapa kuongeza mashambulzii dhidi ya serikali ya Somalia wakati wa mwezi mtukufu wa Ramadan ambao ulianza siku ya Jumatano.
Mapigano makali yaendelea Mogadishu
http://ichef.bbci.co.uk/news/ws/660/amz/worldservice/live/assets/images/2015/04/20/150420095041_somalia_640x360_epa.jpg
Mapigano makali yaendelea Mogadishu
Mapigano makubwa yameripotiwa kwenye mji kuu wa Somalia Mogadishu baada ya shambulizi la gari la kujitoa mhanga kutokea karibu na makao makuu ya idara ya ujasusi ya nchi hiyo.
Maafisa nchini Somalia wanasema kuwa wapiganaji kutoka kundi la al-Shabab waliingia jengo lililo karibu na makao hayo makuu ya ujasusi, na kukana madai ya al-Shabab kuwa waliingia makao ya ujasusi yenyewe.
Hakuna ripoti zozote zilizotolewa za watu kuuawa au kujeruhiwa
Al-Shabab wameapa kuongeza mashambulzii dhidi ya serikali ya Somalia wakati wa mwezi mtukufu wa Ramadan ambao ulianza siku ya Jumatano.
Saturday, 20 June 2015
neymar apata adhabu ya pigo baada ya kupata kadi nyekundu
Mshambuliaji wa Brazil Neymar atakosa michuano yote ya kombe la Copa America baada ya kupigwa marufuku ya mechi nne.
Mchezaji
huyo wa miaka 23 kutoka kilabu ya Barcelona alionyeshwa kadi nyekundu
kwa kuzozana na wachezaji wa Colombia baada ya Brazil kushindwa na
Colombia 1-0 katika mechi ya makundi.Lakini shirikisho la soka la Marekani ya kusini limekiangazia tena kisa hicho na kuongeza adhabu hiyo.
Vyombo vya habari vya Brazil vinasema kuwa alimkaripia refa kabla ya kuingia katika chumba cha mapumziko.
maafisa 15 wa usalama wauwawa na al shabab . hawa jamaa ni hatari sana
Wanamgambo wamewaua karibu walinda usalama 15 nchini Somalia baada ya
kufanya shambulizi katika mji ulio karibu na mji mkuu Mogadishu.
Maafisa
wanasema kuwa wanamgambo wa Al Shabaab kwanza walishambulia kizuizi cha
polisi cha Afgoye ambapo waliwaua polisi watatu na kuchukua magari
kadha.Kisha waliwavamia na kuwaua wanajeshi kadhaa.
Al Shabaab wanasema kuwa wameongeza mashambulizi siku za hivi majuzi kwa sababu ni mwezi mtukufu wa Ramadhan.
Friday, 19 June 2015
BAADA YA KUISHA KWA NDOA YAO ONA MALI ZINAVYOPASULIWA NUSU KWA NUSU
Ni kama utani hivi.. eti kweli ikitokea
ndoa inaisha alafu Mahakama ikaamua kila kitu mgawane nusunusu, hiyo
nusu yenyewe ndio inakuwa kwenye mtindo huu??
Der Juli ni
jina la Mjerumani mwingine kwenye Headlines baada ya kuingia mtandaoni
na kutangaza kwamba anauza hivi vitu ambayo wamegawana nusunusu na mkewe
baada ya ndoa kufikia mwishoni.
Cheki pichaz za vitu vyewewe sasa !!
Hapa kuna video wakati jamaa yuko busy kabisa anagawanya vitu
Hii nusunusu unaionaje mtu wangu, iko sawa kweli? Nitafurahi kuona comment yako kwenye haya maamuzi ya mgao mtu wangu !
ona mahali maisha club ilipohamia kwa sasa ,
ni maeneo ya makumbusho pembeni na makumbusho ya taifa yaliyopo kijitonyama .pia ni pembeni ya jengo la millenium tower ambalo watu wengi wanalijua zaidi.
ratiba ya ligi kuu uingereza hii hapa
Ratiba ya mechi za EPL yatolewa
Chelsea
itaanza utetezi wa taji la ligi ya Uingereza wakati itakapoikaribisha
nyumbani Swansea katika wikiendi ya tarehe 8-9 mwezi Agosti.
Manchester
City iliomaliza pointi nane nyuma ya Chelsea itaelekea West Bromwich
huku Manchester United ikikabiliana na Tottenham katika uwanja wa Old
Trafford.Bournemouth iliopandishwa daraja,Watford na Norwich zitakabiliana na Aston Villa,Everton na Crystal Palace mtawalia.
Tuesday, 16 June 2015
list ya wanamichezo wanaolipwa mkwanja mrefu duniani hii hapa maywether akiongoza
Bondia Floyd Mayweather Jr ndio mwanamichezo aliyeingiza pesa nyingi zaidi dunia katika kipindi cha miezi 12 iliyopita kwa mujibu wa jarida la Forbes.
Mayweather ameingiza kiasi cha dola milioni 300 katika kipindi cha miezi hiyo na fedha nyingi ikiwa imepatikana kutoka na pambano lake na bondia Manny Pacquiao.
Manny ameshika nafasi ya pili katika orodha hiyo huku nyota wa kandanda Cristiano Ronaldo akiwa katika nafasi ya tatu kwa wanamichezo waliotengeneza pesa nyingi.
Orodha kamili ipitie katika tovuti ya bbcswahili.com
Ifuatayo ni orodha kamili ya wanamichezo hao
1. Floyd Mayweather, US, US$300m (£194m).
2. Manny Pacquiao, Philippines, $160m (£103.4m)
3. Cristiano Ronaldo, Portugal, $79.6m (£51.4m)
4. Lionel Messi, Argentina, $73.8m (£47.7m)
5. Roger Federer, Switzerland, $67m (£43.3m)
6. LeBron James, US, $64.8m (£41.9m)
7. Kevin Durant, US, $54.1m (£35m)
8. Phil Mickelson, US$50.8m (£32.8m)
9. Tiger Woods, US, $50.6m (£32.7m)
10. Kobe Bryant, US, = $49.5m (£32m)
wakati mataifa ya afrika yanafanya vizuri katka soka eti tanzania tunaweza huu
Michuano ya gofu ya Afrika (African golf Jacket) itakafanyika Windhoek, Namibia huku nchi kadhaa za Afrika ikiwemo Tanzania na Kenya zikitarajiwa kushiriki.
Nchi nyingine ni pamoja na Botswana, Afrika ya Kusini, Zimbabwe, Zambia, Msumbiji, Swaziland na wenyeji, Namibia, ambao watagharamia wageni wao
Makamu wa raisi wa chama cha gofu nchini Tanzania (TGU), Joseph Tango amesema mchezaji Abbas Adamu kutoka Arusha, Kaskazini mwa Tanzania atakuwa ni miongoni mwa washiriki, baada ya kushinda mara mbili michuano iliyopita na akiwa miongoni mwa wachezaji wa daraja la juu (Division A).
Wachezaji wengine wawili watachaguliwa kutoka division B na C na Tango atakuwa kiongozi wa msafara. “Tuna mategemeo wachezaji wetu watafanya vizuri na kurudi nyumbani na ushindi”, amesema Tango.
taarifa kamili ya raheem sterling kuondoka liverpool hii hapa.
Liverpool imekataa ombi la kitita cha pauni milioni 25 na nyongeza ya pauni milioni 5 kutoka kwa Manchester City ili kumnunua Raheem Sterling.
Pia inaaminika kwamba Liverpool inamthamini mchezaji huyo wa miaka 20 kuwa na thamani ya pauni milioni 50 na kwamba haina mpango wa kumuuza .
Mchezaji huyo amehusishwa na mzozo katika uwanja wa Anfield na hivi majuzi alisema kuwa hatoweka sahihi ya mkataba mwengine katika klabu hiyo.
Hatahivyo ajenti wa Sterling Aidy Ward amedaiwa kusema kwamba hatokubali kandarasi nyengine katika klabu ya Liverpool hata akipewa kandarasi ya pauni laki tisa kwa wiki.
Subscribe to:
Posts (Atom)
CAF kumuunga mkono INFANTINO Urais wa FIFA
Shirikisho la soka barani Afrika CAF linamuunga mkono Infantino Rais wa shirikisho la soka barani Africa (CAF) AHMAD AHMAD amesema shir...

-
Tuzo za VMA 2014 zimefanyika na mastaa wengi walifika kwenye hilo tukio. Listi ya mastaa hao iliongozwa na familia ya Jay Z na Beyon...
-
Luca Modric mchezaji bora wa mwaka wa FIFA Wameamua kumpa,ni baada ya kumdhurumu tuzo yake ya msimu wa 2009/10,mwaka huu wameona ai...
-
Mlinda mlango wa Derby Country akipangua mkwaju wa Phil Jones Timu ya DERBY COUNTY inayonolewa na nyota wa zamani wa CHELSEA, FRANK LAM...