Thursday, 19 June 2014

WYNE ROONEY AFUNGA NA KUSHEREKEA GOAL LA KWANZA KUIFUNGIA TIMU YAKE KATIKA KOMBE LA DUNIA LICHA YA TIMU HIYO YA UINGEREZA KUWA KATIKA HATARI YA KUONDOLEWA KATIKA MICHUANO HIYO

Mbio za kuwania ubingwa wa dunia zinazidi kushika,
na hivi punde umemalizika mchezo kabambe
uliowakutanisha Uruguay dhidi ya England.
Matokeo ya mchezo huo ni ushindi wa 2-1 wa
Uruguay.
Luis Suarez akitoka kwenye majeruhi ya goti
ameiwezesha timu kupata ushindi muhimu mbele
ya England.
Suarez alianza kuifungua Uruguay kabla ya Rooney
hajasawazisha, likiwa ndio goli lake la kwanza katika
fainali 3 za kombe la dunia.
England wakiwa na kasi ya kutafuta goli la ushindi,
Suarez tena akawashangaza kwa kufunga goli la pili
kwa mkwaju mkali na mpaka refa anamaliza mpira
Uruguay walikuwa kifua mbele.
Matokeo hayo yanamaanisha England wanakaribia
kuondolewa kwenye mashindano haya, baada ya
kufungwa mechi ya pili., wakipoteza mechi yao
kwanza dhidi ya Italy.
Mpaka sasa timu kubwa za Spain, Australia na
Cameroon zimeshaaga mashindano hayo.

No comments:

Post a Comment

CAF kumuunga mkono INFANTINO Urais wa FIFA

Shirikisho la soka barani Afrika CAF linamuunga mkono Infantino Rais wa shirikisho la soka barani Africa (CAF) AHMAD AHMAD amesema shir...