Tuesday, 17 June 2014

DUNIA INA MAMBO JANANI, MWIMBAJI MMOJA AFANYIWA UPASUAJI HUKU AKIIMBA ILI KUILINDA SAUTI YAKE ISIHARIBIKE.

Mwimbaji Alama Kante, amelazimika kuimba
huku akifanyiwa upasuaji kuondoa uvimbe
kwenye koo lake ili madaktari wasiharibu sauti
yake.
Mwimbaji huyo kutoka Guinea mwenye
makazi yake nchini Ufaransa alipatiwa dawa za
kumfanya asisikie maumivu wala uchungu
wakati wote wa zoezi la upasuaji.
Kante alikuwa akiogopa kupoteza sauti yake
lakini daktari wake alipendekeza afanyiwe
upasuaji huku anaimba.
Kante ambaye kwa sasa amepata nafuu
amesema wakati upasuaji ukiendelea alihisi
kama yuko Senegal na wakati alipoamka na
kuzungumza tena madaktari na wauguzi
walifurahi kwakuwa wametimiza lengo lao.

No comments:

Post a Comment

CAF kumuunga mkono INFANTINO Urais wa FIFA

Shirikisho la soka barani Afrika CAF linamuunga mkono Infantino Rais wa shirikisho la soka barani Africa (CAF) AHMAD AHMAD amesema shir...