Thursday, 27 September 2018

Ronaldo kuivaa Man United

Ronaldo alioneshwa kadi nyekundu dhidi ya Valencia 

Nyota wa timu ya Juventus, Cristiano Ronaldo atacheza mchezo wa ligi ya mabingwa dhidi ya timu yake ya zamani ya Manchester United baada ya shirikikisho la soka barani Ulaya kumpa adhabu ya kukosa mchezo mmoja.

Cristiano Ronaldo alitolewa kwa kadi nyekundu kwenye mchezo wa kwanza wa hatua ya makundi dhidi ya Valencia ya Hispania ambapo Juventus ilishinda kwa bao mbili kwa bila.

Ronaldo atacheza dhidi ya Man Utd baada ya adhabu kupunguzwa

Hiyo ilikuwa kadi nyekundi ya kwanza kwa Ronaldo kwenye michuano hiyo ya Ulaya na kama angeongezewa adhabu na UEFA basi angekosa michezo yote miwili dhidi ya Manchester United.

Kwa maamuzi hayo ya UEFA sasa Ronaldo atakosa mchezo mmoja tu dhidi ya Young Boys ya Uswiss utakaocheza Octoba pili.

No comments:

Post a Comment

CAF kumuunga mkono INFANTINO Urais wa FIFA

Shirikisho la soka barani Afrika CAF linamuunga mkono Infantino Rais wa shirikisho la soka barani Africa (CAF) AHMAD AHMAD amesema shir...