Ligi kuu TANZANIA BARA inaendelea leo ijumaa kwa michezo miwili katika majiji ya TANGA na DSM.
kwenye dimba la Mkwakwani huko jijini Tanga wagosi wakaya COASTAL UNION wanaoshika nafasi ya TISA kwenye msimamo wakiwa na alama TISA watakuwa nyumbani kuwaalika vinara wa ligi hiyo, Mbao FC ya jijini Mwanza wenye aklama 13 mchezo utakaochezwa majira ya saa kumi jioni.
Mchezo wa mwisho utawakutanisha wenyeji AZAM FC waliopo kwenye nafasi ya TANO wakiwa na alama 11 dhid ya wanapaluhengo LIPULI FC ya IRINGA wanaoshika nafasi ya 13 wakiwa wamejikusanyia alama SABA katika michezo MITANO waliyocheza mpaka sasa.
![]() |
Chamazi Complex uwanja wa Azam Fc |
Endapo AZAM FC wataibuka na ushindi watakwea hadi kileleni kwenye msimamo wa ligi kwa kufikisha alama 14 ambazo itakuwa ni alama MOJA dhidi ya MTIBWA SUGAR na MBAO FC wenye alama 13 kila mmoja.
Katika michezo iliyochezwa hapo jana, MTIBWA SUGAR wamepanda hadi kwenye nafasi ya pili kwenye msimamo baada ya kuilaza MWADUI FC kwa bao MOJA kwa BILA katika mchezo uliopigwa kwenye dimba la MANUNGU huko TURIANI.
![]() |
Matokeo ya Michezo miwili iliyochezwa Sept 27 |
Katika mchezo mwingine wazee wa kupapasa RUVU SHOOTING wamefufukua baada ya kuilaza AFRICA LYON kwa bao MOJA kwa BILA lililofungwa na SAID MUSSA kwenye dakika ya 50 ya mchezo huo.
Ushindi huo umeifanya RUVU SHOOTING kufikisha pointi TANO baada ya kucheza michezo SITA na huu ni ushindi wao wa kwanza kwenye msimu huu wa ligi kuu Tanzania Bara.
No comments:
Post a Comment