Thursday, 27 September 2018

EURO 2024 kuchezwa UJERUMANI

Hii ni mara ya kwanza Ujerumani kuandaa michuano ya Euro tangu mwaka 1988
UJERUMANI imeteuliwa kuwa wenyeji wa fainali za kombe la mataifa ya ULAYA (EURO) mwaka 2024 baada ya kuishinda UTURUKI waliokuwa wakiwania nafasi hiyo pia.

Mataifa hayo mawili yaliingia katika kinyang’anyiro cha mwisho kuwania wenyeji huo kabla ya kura zilizopigwa mjini NYON nchini USWISS yalipo makao makuu ya shirikisho la soka barani ulaya UEFA ambao UJERUMANI wameibuka kidedea.

Nahodha wa zamani wa Ujeruman Philip Lahm ameteuliwa kuwa balozi wa michuano hiyo

Wenyeji huo unamaana kuwa kwa mara ya kwanza UJERUMANI itahodhi mashindano ya ulaya kama taifa MOJA baada ya iliyokuwa UJERUMANI MAGHARIBI kuandaa fainali kama hizo mwaka 1988 huku UTURUKI ikisalia bila kuandaa mashindano yoyote makubwa ya mpira katika historia yao.

Ujerumani waliomba kuanda michuano hiyo mwaka 2008, 2012, 2016 bila mafanikio

Kabla ya kupata wenyeji huo UJERUMANI iliwahi kuomba kuandaa faionali za EURO mwaka 2008, 2012 na 2016 ambako zote hawakufanikiwa lakini pia waliomba kuandaa michuano ya OLYMPIC ya mwaka 2020 ambayo nayo hawakufanikiwa baada ya kuzidiwa na JAPAN na walifanikiwa kuwa wenyeji wa fainali za kombe la FIFA la duinia za mwaka 2006.

VAR kutumika ligi ya mabingwa ulaya


Shirikisho lao soka barani Ulaya (UEFA) limesema litaanza kutumia Maamuzi ya msaada wa video (VAR) kwenye michuano ya ligi ya mabingwa barani Ulaya kwenye msimu wa 2019-2020.

Rais wa UEFA, Aleksander Ceferin amesema shirikisho lake litakuwa na mfumo ila wa kutumia VAR ili iweze kutenda haki kwa kila mtu pia watatoa mafunzo ya uhakika kwa waamuzi wote ili waweze kuelewa mfumo huo wa VAR.

Pia VAR itatumika kwenye mchezo wa Super Cup na michuano ya Ulaya ya mwaka 2020 pamoja na michuano ya Europa kwenye msimu wa 2020-2021.

VAR ilikuwa kivutio kwenye kombe la dunia huko Russia

Mfumu  wa kutumia msaada wa video  kutoa maamuzi hasa ya utata yalivutia wengi kwenye michuano ya kombe la Dunia ya mwaka huu iliyofanyika nchini Russia na ligi kubwa barani Ulaya zinatumia mfumo huo isipokuwa ligi kuu ya England.

Ronaldo kuivaa Man United

Ronaldo alioneshwa kadi nyekundu dhidi ya Valencia 

Nyota wa timu ya Juventus, Cristiano Ronaldo atacheza mchezo wa ligi ya mabingwa dhidi ya timu yake ya zamani ya Manchester United baada ya shirikikisho la soka barani Ulaya kumpa adhabu ya kukosa mchezo mmoja.

Cristiano Ronaldo alitolewa kwa kadi nyekundu kwenye mchezo wa kwanza wa hatua ya makundi dhidi ya Valencia ya Hispania ambapo Juventus ilishinda kwa bao mbili kwa bila.

Ronaldo atacheza dhidi ya Man Utd baada ya adhabu kupunguzwa

Hiyo ilikuwa kadi nyekundi ya kwanza kwa Ronaldo kwenye michuano hiyo ya Ulaya na kama angeongezewa adhabu na UEFA basi angekosa michezo yote miwili dhidi ya Manchester United.

Kwa maamuzi hayo ya UEFA sasa Ronaldo atakosa mchezo mmoja tu dhidi ya Young Boys ya Uswiss utakaocheza Octoba pili.

UJERUMANI itashinda kombe la dunia - LOW

Kocha wa Ujerumani Joachim Low
Kocha wa timu ya taifa ya UJERUMANI, JOACHIM LOW anasema kikosi cha DFB kinauwezo wa kushinda tena kombe la FIFA la dunia baada ya morali kurejea ndani ya timu hiyo.

Mabingwa hao wa dunia mwaka 2014 waliishia katika hatua ya makundi kwenye fainali za kombe la FIFA la dunia mwaka huu kule nchini RUSSIA baada ya kutandikwa mabao MAWILI kwa BILA na KOREA KUSINI.

Ujerumani waliondolewa katika hatua ya makundi kombe la dunia 2018

LOW anasema wakati Fulani walikosa hamasa waliyokuwa nayo huko nyuma huku baadhi ya wachezaji wakiwa nje ya kiwango chao kitendo kilichowashangaza na wamejifunza kutokana na hilo na wamelifanyia kazi.

LOW aliajiriwa kukinoa kikosi cha UJERUMANI mwaka 2006 na kabla ya kuanza kwa fainali za kombe la FIFA la dunia kule RUSSIA aliongezewa kandarasi mpya itakayomfanya kuhudumu katika wadhifa huo hadi mwaka 2022 katika fainali za kombe la FIFA la dunia kule nchini QATAR.

Ujerumani walishinda kombe la dunia mwaka 2014

Mbali na kuiongoza UJERUMANI kushinda kombe la FIFA la dunia mwaka 2014 kocha huyo pia alikiongoza kikosi hicho kufika fainali ya kombe la mataifa ya ulaya mwaka 2008 na mwaka 2010 waliishia katika hatua ya nusu fainali kwenye fainali za kombe la FIFA la dunia hatua aliyowaongoza kufika katika fainali za Euro za mwaka 2012 na 2016.

RAMSEY kutimka ARSENAL

Aaron Ramsey akitekeleza majukuma yake uwanjani
Kiungo wa ARSENAL, AARON RAMSEY huenda akatimka katika klabu hiyo baada ya mazungumzo ya kumuongezea kandarasi mpya kugonga mwamba.

Mazungumzo kati ya mchezaji huyo na mabosi wa ARSENAL juu ya kandarasi mpya ya miaka MINNE awali yalielezwa kufikia pazuri lakini saa chache kabla ya kutiliwa saini ARSENAL walijitoa.

 Mkataba wa sasa wa RAMSEY na ARSENAL unafikia tamati JUNE 30 mwakani ambapo mchezaji huyo atakuwa huru au ARSENAL waamue kumuuza mwezi JANUARY kama wanataka kupata chochote kutoka mchezaji huyo.

Ramsey aliifungia Arsenal goli la ushindi kwenye fainali ya FA Cup 2017 dhidi ya Chelsea

Pamoja na yote hayo kiungo huyo wa kimataifa wa WALES atakuwa huru kuingia makubaliano yoyote ya awali na klabu nyingine kuanzia mwezi JANUARY mwakani kwani mkataba wake utakuwa umebakiza miezi sita ambayo kisheria unaruhusiwa kufanya makubaliano na timu nyingine.

RAMSEY alijiunga na GUNNERS mwaka 2008 kwa kitita cha paundi milioni 4.8 akitokea CARDIFF CITY na ndiye mchezaji wa ARSENAL aliyehudumu kipindi kirefu na kufunga bao la ushindi katika fainali ya kombe la FA mwaka 2017 dhidi ya CHELSEA.

Ramsey alijiunga na Arsenal mwaka 2008 akitokea Cardiff City akiwa na miaka 17

Hata hivyo RAMSEY alikuwa mchezaji wa ziada katika ushindi wa ARSENAL wa mabao MATATU kwa MOJA dhidi ya BRENTFORD kwenye kombe la CARABAO siku ya Jumatano ambapo aliingia kwenye dakika ya 84 kitendo kilichoongeza maneno kuwa huenda akatimka.

AJIB, KICHUYA na NYONI wakatwa STARS

Kocha wa Taifa Stars Emanuel Amunike
Kocha Mkuu wa Timu ya Taifa ya Tanzania "Taifa Stars" EMMANUEL AMUNIKE ametangaza kikosi cha wachezaji 30 watakaoingia kambini Septemba 30 kujiandaa na mchezo wa kufuzu fainali za Africa dhidi ya CAPE VERDE. 

Katika kikosi hicho Kocha AMUNIKE amewaongeza wachezaji watano (5) kutoka kwenye kikosi cha awali ambao ni JONAS MKUDE, SHOMARI KAPOMBE, na JOHN BOKO kutoka SIMBA pamoja na FEISAL SALUM wa YANGA na ABDALLAH KHERI wa AZAM FC.

Mlinzi wa mkongwe Erasto Nyoni hajaitwa kikosi cha Stars

Amunike hajawajumuisha beki ERASTO NYONI na viungo SHIZA KICHUYA wa SIMBA na IBRAHIM AJIB wa YANGA katika kikosi chake cha wachezaji 30 kuelekea mechi hizo mbili za kufuzu Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) dhidi ya CAPE VERDE.

Taifa Stars watakuwa wageni wa CAPE VERDE katika mchezo wa Kundi L wa kuwania kufuzu kwa fainali za AFCON Oktoba 12 mjini PRAIA kabla ya kurejea Dar es Salaa kwa mchezo wa marudiano na wapinzani wao hao utakaopigwa Oktoba 16 kwenye dimba la taifa.

Ibrahim Ajib amekuwa na kiwango bora sana msimu huu lakini hajaitwa timu ya taifa


Kwa kiasi kikubwa kocha huyo MNIGERIA ameita wachezaji waliomsaidia kupata sare ya ugenini Septemba 8 mjini KAMPALA dhidi ya UGANDA.

Tanzania inashika nafasi ya tatu katika Kundi L ikiwa na pointi mbili baada ya kutoka sare katika mechi zake mbili za mwanzo, wakitoka 1-1 na Lesotho nyumbani mwaka jana na 0-0 na Uganda ugenini mapema mwezi huu.

Kiungo msumbufu na mnyumbulifu Shiza Kichuya ameachwa Stars

Uganda wanaendelea kuongoza Kundi hilo kwa pointi zao nne, wakifuatiwa na Lesotho wenye pointi mbili sawa na Tanzania na mabao mawili ya kufunga, wakati Cape Verde wanashika mkia wakiwa na  pointi yao moja. 

Kihistoria Tanzania imecheza fainali moja tu za AFCON, mwaka 1980 nchini Nigeria, enzi hizo zikijulikana kama Fainali za kombe la Mataifa Huru ya Afrika. 

AZAM FC, WAGOSI WA KAYA Kukinukisha leo


Ligi kuu TANZANIA BARA inaendelea leo ijumaa kwa michezo miwili katika majiji ya TANGA na DSM.

kwenye dimba la Mkwakwani huko jijini Tanga wagosi wakaya COASTAL UNION wanaoshika nafasi ya TISA kwenye msimamo wakiwa na alama TISA watakuwa nyumbani kuwaalika vinara wa ligi hiyo, Mbao FC ya jijini Mwanza wenye aklama 13 mchezo utakaochezwa majira ya saa kumi jioni.

Mchezo wa mwisho utawakutanisha wenyeji AZAM FC waliopo kwenye nafasi ya TANO wakiwa na alama 11 dhid ya wanapaluhengo LIPULI FC ya IRINGA wanaoshika nafasi ya 13 wakiwa wamejikusanyia alama SABA katika michezo MITANO waliyocheza mpaka sasa.

Chamazi Complex uwanja wa Azam Fc

Endapo AZAM FC wataibuka na ushindi watakwea hadi kileleni kwenye msimamo wa ligi kwa kufikisha alama 14 ambazo itakuwa ni alama MOJA dhidi ya MTIBWA SUGAR na MBAO FC wenye alama 13 kila mmoja.

Katika michezo iliyochezwa hapo jana, MTIBWA SUGAR wamepanda hadi kwenye nafasi ya pili kwenye msimamo baada ya kuilaza MWADUI FC kwa bao MOJA kwa BILA katika mchezo uliopigwa kwenye dimba la MANUNGU huko TURIANI.

Matokeo ya Michezo miwili iliyochezwa Sept 27

Katika mchezo mwingine wazee wa kupapasa RUVU SHOOTING wamefufukua baada ya kuilaza AFRICA LYON kwa bao MOJA kwa BILA lililofungwa na SAID MUSSA kwenye dakika ya 50 ya mchezo huo.

Ushindi huo umeifanya RUVU SHOOTING kufikisha pointi TANO  baada ya kucheza michezo SITA  na huu ni ushindi wao wa kwanza kwenye msimu huu wa ligi kuu Tanzania Bara.

Tuesday, 25 September 2018

MUPE,MURUKEE,MUPEE,MURUKEEE,MURUKEEEE......!!!!!!



Luca Modric mchezaji bora wa mwaka wa FIFA
Wameamua kumpa,ni baada ya kumdhurumu tuzo yake ya msimu wa 2009/10,mwaka huu wameona aibu.
Labda walimruka kwa makusudi ili watengeneze ushindani wa Lionel Messi na Cristiano Ronaldo uliodumu kwa miaka kumi.

Alikuwa kwenye kiwango bora kabisa cha kuweza kutwaa tuzo ya mchezaji bora wa dunia,lakini kwa kuwa jina lake lilikuwa haliuzi kutokana na klabu na ligi aliyokuwa akiichezea kwa wakati huo,wakaamua kumnyima kwa makusudi"a world is not fair at all"(dunia haina usawa kabisa).

Kitita cha Euro milion 15 (€15m) kilimng'oa Estadio Santiago Bernabeu na kuelekea Giuseppe Meazza kule jijini Milan kumpisha mfalme wa Rossoneri,aliyeacha alama kwenye dimba la San Siro,Ricardo Izecson Dos Santos Leite,Kakà.

Hakukawia kuingia kwenye mfumo wa Jose Mourinho.Nguvu ,stamina na nishati yake uwanjani vilimtofautisha na wachezaji wengi wa nafasi yake uwanjani,akiigawa mipira kwa staili anayoitaka yeye,yaan "mupe,murukee,mupee,murukee,murukee,mupeeee" kama muhudumu wa bar anayewahudumia wateja wake.
Ricardo Kaka mwanasoka bora duniani mwaka 2007

Wesley Benjamin Sneijder,mchezaji wa kimataifa wa Uholanzi aliyemnyima usingizi babu Sir Alex Ferguson wakati wa siku za neema za Manchester United,akiisaka sahihi yake usiku na mchana bila mafanikio.

Msimu wake wa kwanza kutua "Nerazzuri" ,aliisaidia Inter Milan kuchukua makombe makubwa matatu waliyoshiriki.Walichukua ubingwa wa ligi kuu nchini Italia "Serie A" maarufu kama Scudetto,walichukua kombe la Coppa Italia na kisha wakachukua ubingwa wa klabu bingwa barani Ulaya (UCL).

Katika nusu fainali ya klabu bingwa barani Ulaya,Inter Milan walikutana na mabingwa watetezi FC Barcelona,Sneijder aliwaonesha "Italian Job" viungo wa Barcelona waliounda sambusa yao iliyowekwa nta na Lionel Messi,Xavi Hernandez na Andres Iniesta huku Sergio Busquet akiishikilia vyema isianguke na kuingia mchanga.Matokeo ya jumla ya michezo yote miwili,Inter Milan aliingia fainali kwa jumla ya magoli 3-2.

Fainali ikapigwa Santiago Bernabeu,maskani ya pepo ya Sneijder iliyogeuka jehanamu kwake kutokana na ujio wa "Magalacticos " kama Cristiano Ronaldo na Ricardo Kaká.

Sneijder kama kawaida yake awapo uwanjani,akawa anatawanya mipira kuwalisha Diego Milito na Samuel Eto'o kwa mtindo ule ule wa MUPE,MURUKEE,MUPEE,MURUKEE,MURUKEE.Inter Milan wakawafunga Bayern Munich magoli 2-0 huku Sneijder akitoa "assist" moja kati ya magoli hayo yaliyofungwa na Diego Milito.

Wesley Sneijder licha ya kucheza kwenye kiwango cha juu sana hakuwahi kushinda tuzo

Sneijder akatua bondeni kwenye kombe la dunia,akaendeleza wimbi lake la kutawala eneo la kati,safari hii sio kuisaidia timu yake kufuzu kwa kushinda mechi zote nane za makundi,bali aliwapitisha salama kwenye bonde la uvuli na mauti ya soka kwa kuwafungia magoli matano kwenye michuano hiyo,mawili yakiwa dhidi ya "Selecao wa Brazil",na kumaliza mashindano wakiwa washindi wa pili na yeye kuwa na idadi sawa ya magoli na Thomas Müller,mfungaji bora wa Mashindano hayo.

Wakati yanatajwa majina matatu ya wachezaji wanaowania tuzo ya mchezaji bora wa FIFA wa dunia (Ballon d'Or) kipindi hicho,jina la kiungo Wesley Sneijder halikuwemo kwenye orodha hiyo,yaan wali-mupa Xavi waka-muruka Sneijder,waka-mupa Iniesta na KUMUPA tuzo hiyo Lionel Messi.

Baada ya hapo tuzo ikawa inahama kwa mtindo wa upatu,yaan nipe nikupe kati ya Messi na Ronaldo,inatoka Madrid inaenda Madeira kusalimia,ikitoka huko inarudi tena Hispania kwenye jimbo la Katalunya na kuelekea Rosario kupiga " selfie" na washkaji,hakuna upinzani.

Siku zikapita,ikawa mchana ikawa asubuhi,majira yakasogea,Uholanzi wakapotea kwenye Ulimwengu wa soka,Sneijder akatangaza kung'atuka kwenye soka la kimataifa,akatuachia mrithi wa kazi yake,naye ni Mtakatifu machoni pa wanandinga wengi duniani,Luka Modric wa Real Madrid na timu ya taifa ya Croatia.

Luca Modric akiipigania jezi ya Croatia

Mchezaji wa nafasi ya kiungo.
Nafasi aliyokuwa anacheza Sneijder wakati yupo Madrid ndio nafasi anayocheza Modric leo hii,namba ya jezi aliyoshinda nayo UEFA Sneijder ndio namba ya jezi aliyoshinda nayo Modric na kumpa tuzo ya mchezaji bora wa dunia.

Mafanikio ya timu zao za taifa kati ya wawili hao kwenye kombe la dunia yote ni sawa,wote walishika nafasi ya pili,japokuwa Modric alimaliza na magoli mawili lakini Sneijder alimaliza na magoli matano na hakupata tuzo yoyote,FIFA walimruka....MUPE,MURUKE,MUPEE,MURUKEE,MURUKEEE........!!!!

Huko alipo najua Sneijder anafurahia tuzo ya Modric,anajihisi ni kama ameipata yeye,kwani vigezo vilivyompa tuzo Modric ndivyo hivyo hivyo vilivyomnyima Sneijder,ama kweli dunia haina usawa...!!

Luca Modric akiwa kibaruani na jezi ya Real Madrid

Kitu pekee cha kujivunia kwa Sneijder ni ile huduma ya "free delivery" ya mipira aliyokuwa anaifanya uwanjani,sasa imepata mrithi sahihi ambaye ni Luka Modric na kutambuliwa mchango wake,anakupa akitaka,anakuruka asipotaka,na anafunga kwa mateso makali kama alivyomning'iniza Willy Caballero wa Argentina kwenye kombe la dunia.

@Sir_Rwechu
©2018

HAMILTON jino kwa jino na VETTEL katika RUSSIAN GRAND PRIX

Lewis Hamilton anaongoza kwa tofauti ya alama 40 dhidi ya Sebastian Vettel 
Kuelekea mbio za Langalanga za RUSSIAN GRAND PRIX zitakazofanyika mjini SOCHI jumapili hii kampuni ya MERCEDES imesema haitabweteka licha ya dereva wake LEWIS HAMILTON kuongoza kwa alama 40 mbele ya mpinzani wake mkubwa SEBASTIAN VETTEL katika msimamo wa mbio hizo.

HAMILTON ameshinda mashindano MATATU kati ya MANNE yaliyopita na kujikusanyia jumla ya alama 281 akiwa kinara na kampuni ya FERARI chini ya dereva wake mashuhuri SEBASTIAN VERTEL anayeshika nafasi ya pili akiwa na alama 241 wana kibarua cha kupindua matokeo katika mashindano SITA yaliyosalia ambayo yana jumla ya alama 150.

Mtendaji mkuu wa MARCEDES, TOTO WOLFF anasema ni jambo jema kwao kuongoza msimamo mpaka hivi sasa na kwamba wapinzani wasifikiri kuwa watalegeza kamba na badala yake wataendelea kupambana zaidi.

Marcedes wanaimani kubwa ya kutetea taji la dunia

WOLFF anasema kampuni ya MERCEDES ilishangazwa na jinsi madereva wake walivyopambana katika mashindano SITA yaliyopita na kusisitiza kuwa sasa wanaweka umakini zaidi kwenye kila shindano lililkosalia ikiwemo kuhakikisha gari zinakuwa kwenye ubora wakati wote ili kutetea taji la dunaia.

Mbio za langalanga kwa msimu huu zimebakiza mashindano SITA tu kumalizika ambayo ni pamoja na yale yatakayofanyika nchini RUSSIA jumapili hii yakifuatiwa na yale ya JAPANI, MAREKANI, MEXICO, BRAZIL na ABU DHABI.

SINGIDA UTD Vs MBEYA CITY machozi jasho na damu NAMFUA

Singida United kuumana na Mbeya City kwenye dimba la Namfua mjini Singida
Ligi kuu Tanzania Bara inaendelea leo JUMATANO kwa kuchezwa mchezo  mmoja ambapo SINGIDA UNITED waliopo kwenye nafasi ya 14 wakiwa na alama 7 itawaalika wanakoma kumwanya, MBEYA CITY  waliopo kwenye nafasi ya 13 wakiwa na lama 7 pia mchezo utakaochezwa kwenye dimba la NAMFUA mjini SINGIDA.

Katika mchezo pekee uliochezwa jioni ya jana timu ya KMC na LIPULI FC zimeendelea na rekodi yake ya kupata sare kwenye michezo yao ya ligi kuu kwa msimu huu baada ya kutoka suluhu kwenye mchezo uliochezwa kwenye uwanja wa UHURU jijini DSM.


Katika mchezo huo uliokuwa na mashambulizi ya kushitukiza kwa pande zote mbili ulishuhudia mlinzi wa kushoto wa LIPULI FC, PAUL NGALEMA akilimwa kadi nyekundu kwenye dakika ya 90 ya mchezo huo baada ya kumchezea madhambi kiungo wa KMC, CHRIS BUYOYA.

Kwa matokeo hayo timu zote mbili zimefikisha alama SABA ambapo KMC imeshinda mchezo MMOJA na imetoka sare katika michezo MINNE na kupoteza mchezo MMOJA huku LIPULI FC wakishinda mchezo MMOJA na kutoka sare katika michezo MINNE.

LAMPARD Amshangaza MOURINHO Old Trafford

Mlinda mlango wa Derby Country akipangua mkwaju wa Phil Jones
Timu ya DERBY COUNTY inayonolewa na nyota wa zamani wa CHELSEA, FRANK LAMPARD imeitupa nje ya mashindano ya kombe la ligi MANCHESTER UNITED baada ya kuitandika kwa penati 8-7 kufuatia sare ya mabao MAWILI kwa MAWILI kwenye mchezo uliopigwa kwenye dimba la OLD TRAFFORD.

Katika mchezo huo HARRY WILSON amekuwa mchezaji wa kwanza kuifunga MANCHESTER UNITED goli la moja kwa moja la mpira wa adhabu yaani Direct Free Kick katika kombe la ligi kwenye dimba la OLD TRAFFORD tangu alipofanya hivyo GILES BARNES mwezi JANUARY mwaka 2009 wakati akifunga bao la kwanza la kusawazisha kwa DERBY COUNTRY. 

MANCHESTER UNITED imepoteza mechi zake TANO zilizopita katika mashindano yeto ambazo ziliamuliwa na changamoto ya mikwaju ya penati ambapo TATU ni za kombe la ligi, moja kwenye kombe la FA na nyingine kwenye ngao ya jamii.

Derby wamepata ushindi wa kwanza kwenye dimba la Old Trafford tangu mwaka 2001

Mlinda mlango SERGIO ROMERO ni mchezaji wa kwanza wa MANCHESTER UNITED kuoneshwa kadi nyekundu ya moja kwa moja kwenye dimba la OLD TRAFFORD katika mashindano yote tangu alipofanya hivyo mlinzi ERIC BAILLY mwezi MAY mwaka jana 2017 katika mchezo wa ligi ya YUROPA dhidi ya CELTA VIGO baada ya kuoneshwa kadi nyekundu kwenye dakika ya 67.

Wachezaji wa Derby wakishangilia moja ya goli walilowafunga Man Utd

Baadhi ya matokeo mengine ya michezo ya kombe la ligi MAN CITY wakiwa ugenini wameilaza OXFORD UNITED mabao MATATU kwa BILA, WEST BROM wamenyukwa mabao MATATU kwa BILA pia na CRYSTAL PALACE wakati BOURNAMOUTH wakiinyuka BLACKBURN ROOVERS mabao MATATU kwa MAWILI huku BURTON ALBION wakiishangaza BURNLEY kwa kuitandika mabao MAWILI kwa MOJA.

Hii leo kutakuwa na mtanange wa kukata na shoka ambapo majogoo wa jiji LIVERPOOL watakuwa nyumbani kuwakaribisha CHELSEA wakati ARSENAL wakiumana na BRENTFORD huku TOTTENHAM HOTSPURS wakiwakaribisha WATFORD.

Monday, 24 September 2018

Boban achimba mkwara kwa wanaoibeza Lyon

Nahodha wa African Lyon Haruna Moshi amekuwa kwenye kiwango bora msimu huu
Nahodha wa AFRICAN LYON, HARUNA MOSHI maarufu kama BOBAN amesema licha ya kupoteza mchezo dhidi ya MTIBWA SUGAR bado wanaimani kikosi chao kipo kwenye kiwango kizuri kitakachowawezesha kumaliza ligi katika nafasi za juu.

MOSHI anasema timu yao ina mchanganyiko wa wachezaji vijana na wakongwe wenye uwezo wa kupata matokeo wakati wowote hivyo mashabiki wa timu hiyo wasikate tamaa kwani wao kama wachezaji wapo tayari kupambana mpaka tone la mwisho .

Mpaka sasa AFRICA LYON imeshacheza michezo SITA ya ligi kuu msimu huuu ambapo imeshinda mchezo MMOJA na kupoteza michezo MITATU huku ikitoka sare katika michezo MIWILI. 

Modric awabwaga Ronaldo na Salah tuzo za FIFA

Luca Modric ametangazwa mshindi wa tuzo ya mchezaji bora wa kiume wa FIFA katika hafla ilifanyika kwenye ukumbi wa Royal Festival mjini London
Kiungo wa kimataifa wa CROATIA, LUCA MODRIC ameshinda tuzo ya mchezaji bora wa mwaka wa FIFA baada ya kuwashinda CRISTIANO RONALDO na MOHAMED SALAH.

Nyota huyo anayechezea REAL MADRID aliisaidia klabu hiyo kushinda mataji MATATU mfululizo ya ligi ya mabingwa barani ulaya pamoja na kulisaidia taifa lake la CROATIA kufika fainali ya kombe la FIFA la dunia.

Ronaldo na Messi wameshinda tuzo zote kubwa tangu mwaka 2008
Hii ni mara ya kwanza baada ya miaka 10 kupita tuzo kubwa duniani kunyakuliwa na mchezaji tofauti ya RONALDO na MESSI ambapo mara ya mwisho ilikuwa mwaka 2007 pale mbrazil RICARDO KAKA lisposhinda tuzo ya Balon d’or.

Kwa upande wa goli bora la mwaka tuzo imeenda kwa MOHAMED SALAH wa LIVERPOOL ambapo bao lake alilofunga dhidi ya EVERTON mwezi DESEMBA mwaka jana limeteuliwa kuwa goli bora la mwaka.

Salah akifunga goli lililoshinda tuzo ya goli bora la FIFA dhidi ya Everton mwezi Desemba mwaka jana 
Ushindi huo hata hivyo umeibua mjadala hasa kutokana na ubora wa magoli mawili yaliyoshindwa likiwemo goli la CRISTIANO RONALDO dhidi ya JUVENTUS na lile la GARETH BALE dhidi ya LIVERPOOL katika michuano ya ligi ya mabingwa barani ulaya.

Tuzo ya kocha bora wa mwaka imeenda kwa DIDIER DESCHAMP wa UFARANSA aliyewashinda ZINEDINE ZIDANE na ZLADKO DALIC wa CROATIA.

Kocha wa zamani wa Arsena Arsene Wenger akimkabidhi tuzo ya kocha bora Didier Deschamp

 Tuzo ya mchezaji bora wa kike ikienda wa MARTA wa BRAZIL ambaye ameshinda tuzo hiyo kwa mara ya SITA mfululizo. 
Marta mshindi wa tuzo ya mchezaji bora wa kike 

Tuzo ya mashabiki bora ikienda kwa mashabiki wa timu ya taifa ya PERU. Zaidi ya mashabiki arobaini elfu wa Peru walisafiri hadi Russia kuishuhudia timu yao ya taifa ikicheza fainali za kombe la dunia kwa mara ya kwanza baada ya miaka 36.
Mashabiki wa Peru wakiishangilia timu yao huko Russia

Salah na Courtois waachwa kwenye kikosi bora cha FIFA licha ya kutwaa Tuzo katika hafla hiyo
Kikosi bora cha FIFA

Mtibwa Sugar wapania mataji zaidi

Kocha wa Mtibwa Sugar Zuber Katwila
Kocha wa MTIBWA SUGAR, ZUBER KATWILA amesema kama ilivyokuwa msimu uliopita kikosi chake kina malengo ya kunyakua taji mojawapo msimu huu miongoni mwa mashindano wanayoshiriki.

Akizungumza baada ya kumalizika kwa mchezo kati ya MTIBWA na AFRICAN LYON, KATWILA anasema wana kikosi kipana walichokiandaa vyema kwaajili kuwania mataji hivyo anaamini msimu huu hawatatoka patupu. 

Katika mchezo wa jana uliochezwa kwenye dimba la uhuru jijin DSM MTIBWA waliwanyuka wenyeji AFRICAN LYON mabao MAWILI kwa BILA mabao yote yakifungwa na RAJAB ZAHIR na msimu uliopita walifanikiwa kunyakua ubingwa wa michuano ya kombe la shirikisho la soka nchini.

MBAO FC yazidi kutakata Ligi Kuu Bara



Wabishi wa jiji la MWANZA, MBAO FC wamekwea kileleni kwenye msimamo wa ligi baada ya kuibuka na ushindi wa bao MOJA kwa BILA dhidi ya maafande wa jeshi la magereza nchini TANZANIA PRISONS.

Katika mchezo huo ulichezwa kwenye dimba la CCM KIRUMBA timu zote mbili zilitandaza kabumbu safi lakini bahati ilikuwa kwa MBAO ambao walipata bao la ushindi katika daika za lala salama likipachikwa kimiani na NDAKI ROBERT.

Matoke hayo yanawafanya MBAO kufikisha alama 13 baada ya kushuka dimbani mara SITA ambapo wameshinda michezo MINNE na kupoteza mchezo MMOJA huku wakitoka sare katika mchezo MMOJA.

Huko NANGWANDA SIJAONA mjini MTWARA wenye NDANDA FC wamekiona cha moto baada ya kutandikwa mabao MATATU kwa MOJA na chama la wana STAND UNITED matokeo yanayowafanya NDANDA kusalia katika nafasi ya 12 na alama zao SABA huku STAND wakipanda hadi katika nafasi ya NANE wakiwa na alama TISA.

Msimao wa Ligi Kuu baada ya michezo 3 ya jana

#StandingsPPts
1Mbao FC613
2Young Africans SC412
3Azam FC511
4Simba SC510
5Mtibwa Sugar FC610
6JKT Tanzania69
7Coastal Union69
8Stand United FC69
9Biashara United68
10Kagera Sugar FC57
11Mbeya City FC67
12Singida United FC67
13Ndanda FC67
14KMC56
15Lipuli FC46
16African Lyon66
17Tanzania Prisons FC65
18Ruvu Shooting FC52
19Mwadui FC52
20Alliance FC61

CAF kumuunga mkono INFANTINO Urais wa FIFA

Shirikisho la soka barani Afrika CAF linamuunga mkono Infantino Rais wa shirikisho la soka barani Africa (CAF) AHMAD AHMAD amesema shir...